Safari Njema Sept 2017 Safari_Njema_Sept | Page 16

man maish focus things V ipi wasanii. Siwezi complain. Life haijanipeleka mbaya after nduthi yangu kupimpiwa. Wira nimechapa poa na mfuko haikai mbaya. Heshima yangu ya mtaani imerudi form. Sasa Thursday flani niko tu maroundi mwenda mtaa, then nikaska phone ikilia. Kucheki ni manzi flani wa mtaa ambaye ni client loyal. Hadi wa leo sijui ni juju gani nilimwachia. Na ni manzi kitu hadi mtaa watu humwita tortoise. Wadhii base huniambia nirushe lugha hapo, lakini hizo mapressure sipendi. Mimi mtu wa nduthi nitaanzia wapi? Sasa mimi huyo kuelekea kwake. Nikampata akitegea hapo nje kwa gate kama amebebea makaratasi kama thao. Kumchapia ananishow amechelewa auditions. Yeye hudunga wax kwa kampuni ya talent search. Hizo karatasi zilikuwa ni CV za wasanii… alikuwa anafaa kuwa amefika by 9 ngware. Kucheki mtambo ilikuwa already 9.15. Lakini uzuri ni hakuwa anaishia far. Akanidunga morali vile huwa ameniamini na nitamfikisha in the shorest time possible. Mistari kama hizo huwa zinanichangamsha nia je! Nikaseti nduthi vipoa, akadandia, makaratasi ameishikia mbele. Vile nilikuwa nimemcheki alikuwa ha jamaliza kujipanga. Alikuwa bado katika harakai za kuchambua hizo karatasi. Nikamshtua akae chonjo coz airforce iko karibu kupepea. Akanishow ako chonjo tuelekee, lakini sikuskia ni kama amenikamata vipoa. Lakini yeye ni kusema, mimi ni kutenda. Ndo hao sisi teke teke. Kenye napendea Thursday ni vile huwa hakuna jam mwenda kama ya Monday na Tuesday. So tulikuwa teketeke bila pressure. Bado njiani, kidogo kidogo huyo tortoise ashaanza njaro zake za kuchambua karatasi zake. Nikapinduka kumshow aache kuwa mtricky akuwe mpole tufike kwanza. Nikiwa katika hizo harakati za kupinduka, kumbe mbele kuna mlevi anasakata rumba barabarani… wasee kwa barabara kelele wakinishtua nicheki mbele. Kupinduka nacheki mdhii zimemamba kwa barabara. Lakini mi ni yule msee. Nikachapa 1-2 nikamtoka. Hata kabla nijidai, naskia manduru nyuma yangu.. Ala! Kupinduka naoma makaratasi zikipeperuka kila pahali. Kumbe huyo manzi alikuwa ameshtuka akaziachilia. Sasa palikuwa pananyesha makaratasi. Noma ilikuwa karatasi zingine zilimwai jamaa wa nduthi alikuwa nyuma yetu. Sema mdhii kulose control. Sema nduthi kwa kibanda ya mama mboga. Sema mathe kufunikwa na mamboga. Sema jamaa wa nduthi kujipata kwa gunia ya viazi. Noooma sana. Nyuma yangu pia kuna manzi na kelele zake za kupoteza CV za wasanii na kulia vile atachujwa wax. Hiyo sasa ilikuwa kelele ya vuvuzela kwangu. Ameniacha kwa blanda noma na analia vile karatasi zimepepea. Nilikuwa nimejama a je naye. Tuliachana kama tumekatziana, hata siko sure kama atawai panda nduthi yangu tena… Ilinibidi nimeskizana na msee wa nduthi ili hii story isiende mbele. Alikuwa msee mpoa. Hata tumekuwa mabeshte. Mathe naye ilibidi nimelipia mali iliharibika na kumwachia za macho akanyagie hiyo story. Hata nikipitanga hapo tunagoteana na huyo matha vipoa. Mafans, nduthi inaweza kuwa dangerous as much as iko convenient. Focus ni muhimu sana. Kama wee ni abiria focus yako inafaa kuwa kwa safety. Biashara zingine malizia mbele baada ya kufika salama. Tabia ya kubonga na phone, kukata kucha, kusoma vitabu tusare! Pia pilot ni jukumu lako kumake sure abiria wako anafollow safety rules vipoa. Tuicheze safe manze! 16 September 2017